MPAMBANO wa
marudiano kati ya bingwa wa ndondi katika uzani mzito duniani Tyson Fury's
dhidi ya Wladmir Klitscko limethibitishwa kufanyika Oktoba 29 litakalofanyika Ukumbi
wa Manchester.
Fury, 28,
ambaye ni bingwa wa Uingereza, alishinda mataji ya WBO,WBA, na IBF kutoka kwa Klitscko,
40, raia wa Ukraine Novemba mwaka 2015, lakini akajiondoa katika pigano la
marudio lililopangwa kufanyika mwezi Julai kutokana na jeraha la kifundo cha
mguu.
''Ninafurahi
kwamba tutapigana tena. Sasa tuwapatia mashabiki kile walichokitaka,” alisema Meneja
wa Tyson Fury na mjomba wake Peter.




Post a Comment