Picha ya maandalizi ya video ya pili ya wimbo ‘Pale Kati’ aliyoshoot Afrika Kusini
Baraza la Sanaa Taifa (BASATA) limemwita msanii wa muziki wa Hip Hop, Nay wa Mitego ikiwa ni siku chache toka watangaze kuufungia wimbo wake ‘Pale Kati’ kutokana na wimbo huo kudaiwa kukiuka maadili.
Akiongea Jumatatu hii, Nay wa Mitego amesema kwa sasa hawezi kulizungumzia swala la kufungiwa kwa wimbo wake mpaka pale atakapofanya kikao na BASATA.

“Kesho nimeitwa BASATA, nadhani itakuwa ni vizuri nikizungumzanao, alafu ndo nije kuzungumza issue ya kufungiwa,” alisema Nay.
Hapo awali rapper huyo alisema wimbo wa ‘Pale Kati’ utakuwa na video nne tofauti tofauti ambapo mpaka sasa tayari ameshashoot video mbili, moja akiwa ameshoot Afrika Kusini.
Bongo5

Post a Comment

 
Top