MSANII Jose Chameleon anaaminika kuwa mmoja wa wasanii wakubwa wa Afrika Mashariki aliyeupeleke muziki wa Afrika Mashariki kimataifa. Jose ameutawala muziki wa Uganda kwa miaka mingi hadi kufikiwa mahala pa kupewa cheo na kuitwa Dr. Joseph Chameleon.

Hivi karibuni akifanya mahijiano na kituo kimoja cha televisheni nchini Uganda, Jose alikuwa akizungumzia kuhusu muziki wa Afrika Mashariki akafiki sehemu alipoulizwa kama anaamini kuwa Diamond Platnumz kutoka Tanzania ni msanii mkubwa Afrika Mashariki.


Akijibu swali hilo, Chameleon alisema kuwa kuna tofauti kubwa kati ya msanii wa kwenye jukwaa na msanii wa kwenye mitandao na Tv. Alisema Diamond Platnumz sio msanii mkubwa kama wengi wanavyofikiri licha ya yeye kuwa maarufu kwenye mitandao ya kijamii kama Instagram.


Alisema hata alipokuja Uganda, alishindwa kujaza watu kwenye moja ya Club ndogo ya burudani tofauti na yeye akija Tanzania kiasi anaweza kujaza hata uwanja wa mpira.
Jose Chameleon hamtambui Diamond kama msanii mkubwa kwani anaamini yeye ndiye anaeshika usukani wa muziki wa Afrika Mashariki. Alisema Diamond ni msanii anayekuzwa na mitandao ya kijamii na Tv.
CHANZO; Swahilitimes

Post a Comment

 
Top