KOCHA msaidizi wa Simba, Mganda, Jackson Mayanja ametamka kuwa klabu hiyo itaendelea na kambi za kujificha kwa ajili ya kukwepa mbinu zao kuigwa na wapinzani wao ikiwemo Yanga jambo ambalo linaweza kuathiri kiwango chao.
Mayanja pamoja na kocha mkuu wa kikosi hicho cha Simba, Joseph Omog wamejichimbia mkoani Morogoro kwa ajili ya kambi ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.
Mayanja ambaye ni kocha wa zamani wa Coastal Union na Kagera Sugar amesema kuwa, wataendelea kufanya kambi yao kwa usiri mkubwa kwa kuwa hawataki wapinzani wao wafahamu juu ya kile ambacho wanakifanya ikiwa ni pamoja na namna wanavyojiandaa.


“Tunataka tufanye vizuri kwenye msimu ujao hivyo ni lazima kutoweka wazi kila kitu ambacho tutakuwa tunakifanya kama ambavyo tumejichimbia huku kwa ajili ya kuficha mbinu ambazo tutazitumia kwa msimu ujao.
“Unajua kuwa mpinzani wako akikujua jinsi ulivyo inakuwa ni rahisi kwake kukukabili sasa sisi hilo hatutaki litokee na ndiyo maana tunayafanya mambo yetu kwa usiri mkubwa kwa ajili ya kuwafanya maadui zetu wakiwemo wapinzani wetu Yanga wasijue kile tunachokifanya,”alisema Mayanja.

Post a Comment

 
Top