HII sasa ni kufuru kwani mfanyabiashara mkubwa nchini, Mohamed Dewji ‘MO’ amesema yupo tayari kutoa Sh bilioni 20 kuwekeza katika Klabu ya Simba ili ipate mafanikio.
MO alisema ndani ya Sh bilioni 20 atakazotoa, Simba itapata Sh bilioni 5 kwa mwaka, bajeti ambayo itakuwa mara mbili kwa ile ya Yanga ambayo ni Sh bilioni 2.5. Yanga ipo chini ya Mwenyekiti Yusuf Manji ambaye amekuwa akitoa mfukoni kiasi hicho cha fedha.

“Lengo langu ni kuitoa Simba kwenye bajeti ya Sh bilioni 1.2 hadi kufikia Sh bilioni 5 ambazo nitazitoa kila mwaka na kuzizidi Yanga na Azam ambazo zinatumia Sh bilioni 2.5,” alisema MO.

Post a Comment

 
Top