RAIS wa zamani wa Barcelona, Joan Laporta amesema klabu hiyo haimthamini nyota wake Lionel Messi licha ya mafanikio aliyonayo.
Laporta alisema tangu alipoondoka madarakani Messi amekuwa hathaminiwi ndani ya uwanja na rais mpya wa timu hiyo, Josep Maria Bartomeu amedangaya mambo mengi.
Wakati wake tangu alipoingia madarakani mwaka 2003, Laporta alifanikiwa kuiimarisha Barcelona kwa majengo na matokeo mazuri uwanjani kuliko kipindi chochote.

Laporta ameonyesha wazi kutopendezwa na uongozi wa Bartomeu akisisitiza kuwa, unatakiwa kufanya kitu cha ziada ili kuendeleza kipaji cha Messi.
"Klabu haipo katika kiwango cha Messi," alisema Laporta na kuongeza: "Huyu ni mchezaji bora wa kihistoria, ni mchezaji bora wa dunia."
Laporta alisisitiza kwamba,  Bartomeu aliahidi vitu vingi katika kampeni zake mwaka jana lakini vingi hajatimiza hadi leo.

Post a Comment

 
Top