Mchezaji mmoja raia wa Nigeria ametibua mipango ya straika wa zamani wa Azam, Didier Kavumbagu kujiunga na timu moja ya Vietnam.
Kavumbagu alifanya majaribio na timu ya Dong Tan akafuzu, akaomba Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lakini wakati hati yake inafika kwa timu hiyo, jamaa wakawa wamebadili maamuzi kwa kumchukua Mnigeria, ndipo akapelekwa kufanya majaribio timu nyingine ambayo ilimkubali lakini kikwazo kikawa ni ITC ambayo inashikiliwa na Dong Tan na kanuni za Fifa zinasema ni mpaka mchezaji awe amecheza mwaka mmoja ndiyo anaweza kupata ITC nyingine.

Kavumbagu alisema: “Nilifanya majaribio katika timu ya Dong Tan nikafuzu, ajabu wakamsajili mchezaji kutoka Nigeria, nami nikaenda timu nyingine. Sasa Dong walikuwa wameshapewa ITC yangu.
“Ikaonekana kama nimesajili timu mbili lakini haikuwa hivyo, meneja wangu alikasirika sana ila Dong nao wanaona kama wametumia fedha zao bure kwangu, ila mambo yanaenda sawa naweza kucheza Oktoba ligi mpya itakapoanza.”


Post a Comment

 
Top