IMEBAINIKA
kuwa Yanga haikufanya mazoezi ya pamoja ndani ya siku tatu kabla ya kuvaana na
Ndanda jana Jumatano na kutoka nayo sare ya bila kufungana.
Katibu wa
Yanga SC, Baraka Deusdedit amekiri kuwa wachezaji wa timu hiyo hawakufanya
mazoezi siku tatu kabla ya mchezo na Ndanda kutokana na ratiba kubana.
Deusdedit
alisema kwamba kilichotokea ni kocha Mholanzi Hans van der Pluijm aliwapa
mapumziko wachezaji wikiendi (Jumamosi na Jumapili) na bahati mbaya Jumatatu
kukawa na kikao na Mwenyekiti, Manji katika utaratibu wa kawaida wa klabu.
“Kwa hiyo
kama kuna dhana hiyo ya timu kutoa sare jana kwa sababu ya kutofanya mazoezi
siku tatu, benchi la Ufundi litasema katika taarifa yake,” alisema Baraka.
Pamoja na
hayo, Baraka akalalamikia Yanga kupangiwa mechi nyingine ya Ligi Kuu Jumamosi
dhidi ya Maji Maji, wakati jana wamecheza Mtwara.
“Sisi
tumeondoka leo Mtwara, tutafika Dar es Salaam mchana na hatutafanya mazoezi
leo. Kesho ni Ijumaa na keshokutwa Jumamosi tuna mechi nyingine, wakati Simba
waliocheza jana Dar es Salaam wana mechi nyingine Jumapili,”alisema.
Hata hivyo
baada ya sare hiyo benchi la ufundi la Yanga lililalamikia ubovu wa Uwanja wa
Nangwanda Sijaona kuwa hauna viwango pamoja na wachezaji wake kuwa na uchovu.


Post a Comment