KAMA umewahi
kushuhudia mechi yoyote ya Yanga ikimalizika wachezaji wake hufanya nini, basi
taarifa ikufikie wewe kwamba Simba nayo imekuja na mtindo huo lengo likiwa ni
kujiweka fiti zaidi.
Nadhani
unajua, lakini kama hujui ipo hivi, tangu Yanga iwe na kocha msaidizi, Juma
Mwambusi aliyetokea Mbeya City, imekuwa na kawaida ya kufanya mazoezi mepesi
baada ya kumaliza mechi, hali hiyo pia Simba wanayo kwa sasa.
Simba ambayo
kwa sasa inajifua vikali kwenye kambi yao iliyopo mkoani hapa kwa ajili ya msimu
ujao wa Ligi Kuu Bara, tayari imeshacheza mechi tatu za kirafiki dhidi ya
Polisi Moro, Moro Kids na Burkinafaso ambapo mechi hizo zote imeibuka na
ushindi.
Kila baada
ya kumaliza mechi, imekuwa na kawaida ya wale wachezaji waliomaliza mchezo
kunyoosha viungo kabla ya kwenda kupumzika.
Championi
limekuwa likishuhudia hali hiyo kila kwenye mchezo na anayeongoza mazoezi hayo
ni kocha msaidizi, Mganda, Jackson Mayanja hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa
kocha huyo kuitumia staili hiyo.
Post a Comment