KIUNGO
mshambuliaji wa Yanga, Deus Kaseke, amepewa darasa la kuwamaliza Mo Bejaia mara
baada ya kukosekana katika mchezo wa marudiano ya mchezo wa Kombe la Shirikisho
dhidi ya Medeama.
Mchezaji
huyo ambaye amekuwa muhimu kutokana na kasi yake uwanjani akiwa fundi wa
kuanzisha mashambulizi na kuzuia, alikosekana katika mchezo dhidi ya Medeama
kutokana na majeraha yaliyokuwa yakimkabili.
Katika
mazoezi yaliyofanyika katika Uwanja wa Gymkhana jijini Dar es Salaam, kocha
Hans Pluijm alionekana akitengeneza mfumo utakaompa nafasi ya kucheza kwenye
mchezo huo dhidi ya Mo Bejaia.
Kwa upande
wake kocha msaidizi wa timu hiyo, Juma Mwambusi, naye alionekana akimpa
maelekezo mchezaji huyo ambaye alitoka naye katika kikosi cha wagonga nyundo wa
Jiji la Mbeya, Mbeya City.
Kurudi
uwanjani kwa kiungo huyo mshambuliaji
katika kikosi cha kwanza cha vijana wa
Jangwani kutakuwa na faida kubwa
kutokana na uwezo na ubora wake.
Post a Comment