BAADHI ya
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Simba, juzi Jumatatu walivamia kambi ya timu
hiyo na kushuhudia mchezo wa kirafiki kati ya Simba dhidi ya Burkinafaso
inayoshirki Ligi Daraja la Pili Tanzania Bara, huku Chuji na KMC wakiwavaa leo.
Katika
mchezo huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Highland mkoani hapa, ulimalizika kwa
Simba kuibuka na ushindi wa mabao 5-0, ambapo mabosi hao wakiongozwa na katibu
mkuu wa klabu hiyo, Patrick Kahemele, waliushuhudia mwanzo hadi mwisho.
Championi
ambalo nalo lilikuwepo uwanjani hapo, baada ya mchezo huo, liliwashuhudia
Kahemele, Musleh Al Rawah na Frisch Collins wakizungumza na Kocha Mkuu wa
Simba, Joseph Omog raia wa Cameroon.
Hakuna
aliyeweza kusikia wanazungumza nini kwani walikuwa wakiongea kwa siri kubwa,
lakini mazungumzo yao yalichukua takribani dakika 30 mpaka kumalizika ambapo
walionekana kujadili jambo huku wakicheka mara kwa mara.
Hata hivyo,
hakuna kiongozi aliyekubali kuzungumzia kikao hicho kifupi.
Mbali ya
kuwepo kwa viongozi hao waliokuwa wakizungumza na kocha, lakini pia mjumbe
mwingine, Said Tully naye alikuwepo uwanjani hapo, lakini hakuwa sehemu ya
mazungumzo na kocha.
Simba ambayo
imepiga kambi mkoani hapa kwa takribani wiki ya tatu sasa, inatarajiwa kumaliza
kambi yake leo Jumatano kwa kucheza mechi ya mwisho ya kirafiki dhidi ya KMC
kutoka jijini Dar inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, kabla ya kesho Alhamisi
kurudi Dar tayari kwa tamasha lao la Simba Day litakalofanyika Jumatatu ijayo.
Hii itakuwa mara
ya kwanza kwa mashabiki wa soka hapa nchini kumshuhudia kiungo mahiri, Athumani
Idd Chuji akiwa anaitumikia KMC lakini pia akicheza mchezo dhidi ya timu yake
ya zamani Simba.
Post a Comment