Angban

KIPA namba moja wa Simba, Muivory Coast, Vincent Angban, ametamka kuwa kuja kwa kipa mwingine ndani ya timu hiyo, Mwadini Ali kutampa changamoto ya namba mara baada ya kukosa upinzani mbele ya kipa mwenzake Peter Manyika jambo ambalo lilimfanya kutumika yeye kwenye sehemu kubwa ya msimu uliopita.
Viongozi wa Simba wamemjumuisha Mwadini Ali kutoka Azam katika kikosi chao cha msimu ujao ambapo kipa huyo ametua sambamba na mshambuliaji Ame Ali ‘Zungu’ ambapo wote wapo kwa mkopo.
Angban amesema kuwa hana shaka yoyote na ujio wa Mwadini katika kikosi hicho kwa kuamini kuwa atamfanya kiwango chake kikue zaidi ya msimu uliopita.
 Mwadini

“Kuja kwake Mwadini hapa Simba ni jambo zuri kwetu kwa sababu tumezidi kuwa makipa wengi wenye viwango vikubwa pamoja na uzoefu na jambo hilo naamini litatusaidia kuifanya timu ipate mafanikio zaidi.
“Lakini kwangu pia naamini atanipa msaada wa kuinua kiwango changu kwa sababu mwanzo nilikosa mpinzani halisi lakini kwa hapa nitakuwa makini kwa kuonyesha uwezo kwani najua nisipofanya hivyo yeye atajituma na kuchukua namba yangu,” alisema Angban.


Post a Comment

 
Top