MSHAMBULIZI wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ na klabu ya Yanga SC, Jerson Tegete amethibitisha kuwa ataachana na Mwadui FC baada ya kumalizika kwa mkataba wake wa mwaka mmoja.

Tegete mshindi wa mataji manne ya ligi kuu (2008/09, 2010/11, 2012/13, 2014/15) alijiunga na Mwadui ya Shinyanga mwaka mmoja uliopita akiwa chini ya Kocha Jamhuri Kiwhelo ‘Julio’.

“Ni kweli nimemaliza mkataba wangu na Mwadui. Nitaondoka katika timu hiyo,” anasema Tegete nilipofanya naye mahojiano mafupi siku ya Jumatano hii.

Mshambulizi huyo alicheza kwa miaka saba katika kikosi cha Yanga na ni kati ya washambuliaji wawili waliopata kufunga magoli mengi katika historia ya ‘Dar es Salaam derby’ sambamba na Emmanuel Gabriel waliofunga magoli matano kila mmoja.

Msimu uliopita alifunga magoli matano tu katika VPL na kuwa kinara wa ufungaji katika timu yake.

“Nipo katika mazungumzo na baadhi ya timu, soon nitawaambia ni timu gani nitachezea msimu ujao. Itakuwa ni timu ya hapa nyumbani,” anasema Tegete ambaye ni mmaliziaji aliyetajwa ‘mviziaji wa kiwango cha juu.’
Chanzo: Shafiidauda

Post a Comment

 
Top