KIKOSI cha Tanzania Prisons kinachonolewa na Kocha, Salum Mayanga kimeripotiwa kupata mrithi wa aliyekuwa kipa wao tegemeo, Beno Kakolanya, kwa kumsainisha kipa wa zamani wa Simba na Kagera Sugar, Andrew Ntala.
Prisons ambayo maskani yapo mkoani Mbeya  tayari imewapoteza nyota wake wawili tegemeo ambao ni Kakolanya na Mohammed Mkopi aliyetua kwa majira zao Mbeya City baada ya mkataba wake na Wajelajela hao kumalizika.
Nyota wengine walioungana na Ntala kutia saini ni Samatta ambaye aliwahi kucheza Mgambo Shooting.

Post a Comment

 
Top