BENCHI
jipya la ufundi la Azam FC linaloongozwa na Wahispania watano na Mbongo, Denis
Kitambi, limekuja na falsafa ya kipekee kikosini hapo, baada ya kutangaza
kufuta usajili wa kikosi kizima na kuanza moja kabisa kusaka wachezaji wengine.
Benchi
hilo lililo chini ya Kocha Mkuu Zeben Hernandez akisaidiana na Wahispania
wenzake wanne wote kutoka Tenerife ya nchini kwao, limetoa msimamo huo ikiwa na
maana hata wachezaji mastaa wa kikosi hicho, John Bocco na Kipre Tchetche nao
wanalazimika kuonyesha uwezo ili wapate namba.
Makocha
wengine ni kocha msaidizi Yeray Romero, Pablo Borges (kocha wa makipa) na kocha
wa viungo, Jonas Garcia.
Azam
ilianza rasmi mazoezi jana Alhamisi katika uwanja wao wa Chamazi Complex ambapo
pia wale waliokuwa kwa mkopo msimu uliopita kama Kelvin Friday (kutoka Mtibwa),
Omar Wayne (Coastal Union) na Joseph Kimwaga (Simba) nao wakiwa mazoezini.
Msemaji
wa kikosi hicho, Jaffar Idd Maganga ameliambia Championi Ijumaa kuwa, kocha
alitoa pendekezo ya kuanza na moja kwani benchi zima haliwajui wachezaji wao,
hivyo kutoa nafasi ya kukiangalia upya kikosi kwa muda wa siku 15 kabla ya
kutangaza akina nani watasalia kikosini.
“Kwa
sasa kila mmoja ana nafasi ndani ya Azam na baada ya muda mwalimu alioomba
(siku 15) ndipo tutajua Azam ya msimu ujao itakuwa na wachezaji aina gani,”
alisema Idd.
Kipre matatani Azam
Idd
aliongeza kuwa wanafanya kila njia kupata sababu za mshambuliaji wao, Muivory
Coast, Kipre Tchetche kutorejea kikosini mpaka jana kinyume na taratibu ambapo
alitakiwa kuwa kikosini.
“Kipre
bado ni mchezaji wetu, ana mkataba wa mwaka mmoja hivyo hawezi kwenda popote na
bahati nzuri hata ITC yake tunayo sisi, kwa hiyo tunajaribu kufanya mawasiliano
kujua sababu ya kuchelewa kambini na kinyume cha hapo atachukuliwa hatua,”
alisema Idd.
Naye
pacha wa nyota wa Kipre, Michael Bolou alipoulizwa na gazeti hili kuhusu
alikomuacha mwenzake alijibu kwa kifupi: “Mimi nilimuacha nyumbani, mengine
sifahamu lolote.”
Post a Comment