UONGOZI wa Klabu ya Simba umeshtukia janja ya mahasimu wao Yanga ya kutaka kumsajili beki wake wa kushoto, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’ ambaye inadaiwa tayari wameshaanza kufanya naye mazungumzo ya kutaka kuvunja mkataba, hivyo uongozi huo umeamua kumuongeza mkataba mwingine.

Tshabalala ni beki aliyeonyesha uwezo mkubwa msimu uliopita licha ya timu yake kuyumba mara kadhaa, hali ambayo ilisababisha Yanga ionyeshe nia ya kumsajili na tayari kulikuwa na taarifa kuwa imeanza mipango rasmi ya kutekeleza jukumu hilo.

Akizungumza na Championi Ijumaa, beki huyo alisema taarifa za Yanga kumhitaji amezisikia huku akidai kuwa bado ana mkataba na Simba na tayari wameanza mazungumzo naye ya kumuongezea mkataba mpya ili Yanga walimpate.

“Mimi ni mchezaji halali wa Simba na tayari kuna mazungumzo mapya ya kuongeza mkataba mwingine lakini sijajua utakuwa wa muda gani.

“Moja ya malengo niliyojiwekea ni kuhakikisha napata nafasi ya kucheza nje ya nchi, hivyo mtazamo wangu haupo kwenye kutua Yanga wala timu yeyote ya hapa Bongo mara baada ya kumalizana na Simba nahitaji kucheza nje,” alisema beki huyo.

Post a Comment

 
Top