LICHA ya kutoka sare ya bao 1-1 na Medeama, Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm amesema ana imani kubwa kikosi chake hicho kitatinga nusu fainali ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga ambayo ina alama moja baada ya kushuka dimbani mara tatu, kimahesabu bado ina nafasi kwani ina mechi tatu na kati ya hizo moja inacheza nyumbani hivyo ikipata ushindi kwenye michezo hiyo inaweza kutinga hatua inayofuata.
Pluijm alisema vijana wake walipambana katika mchezo wa jana lakini bahati haikuwa yao kwani walishindwa kuzitumia nafasi walizozipata.
"Ukiniuliza kuwa tunaweza kufuzu katika hatua ya nusu fainali jibu lake ni ndiyo kwakuwa katika mpira kila kitu kinawezekana,tumebakiwa na mechi tatu na tukishinda zote tutakuwa na alama kumi," alisema Hans.
Naye Kocha wa Medeama, Pride Yaw Owusu alisema Yanga walicheza vizuri lakini wao lengo lao lilikuwa ni kupata pointi moja ambayo walifanikiwa kuinyakua.

Baada ya matokeo ya jana kundi lao lipo hivi:
CAF Confederation Cup
Group A
                                    P      W     D      L       Pts
1      TP Mazembe      2      2      0         0      6
2      Mo Bejaia           2      1      1        0      4
3      Medeama           3      0      2        1      2
4      Yanga                 3      0      1        2      1

Post a Comment

 
Top