Nchini Rwanda kwenye uwanja wa Amahoro jijini Kigali leo kulikua na pambano la fainali ya kombe la Amani kati ya watani wa jadi wa Rwanda timu ya jeshi APR na RAYON SPORTS.
Pambano hilo limemalizika kwa RAYON SPORTS kufuta uteja wa kufunwa mara kwa mara na APR baada ya kuifunga timu hiyo ya jeshi la ulinzi la Rwanda bao 1 kwa bila mbela ya maelfu ya mashabiki walikua wamefurika kwenye uwanja huo.
Mchezaji Ismaila Diara kutoka Mali ndiye aliyefunga goli hilo katika dakika ya 3 kati ya zile 4 za nyongeza baada ya dakika 90 kutimia.

Mara ya mwisho kwa RAYON SPORTS kuifunga APR kwenye mchezo wa fainali wa kombe la Amani ilikua ni mwaka 2010 pale mchezaji marehemu Patrick Mutesa Mafisango alipofunga bao pekee kabla ya kuhamia klabu ya Simba ya Tanzania.
Kufuatia ushindi huo, RAYON SPORTS wamekabidhiwa kombe lao mbele ya mke wa rais wa Rwanda Janeth Kagame na maafisa wa shirikisho la soka la nchi hiyo FERWAFA na wataiwakilisha nchi kwenye michuano ya kombe la Shirikisho Barani Afrika mwakani.

Post a Comment

 
Top