AFYA ya Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara imezidi kuwa tete na sasa anatarajiwa kwenda nje ya nchi kwa matibabu zaidi baada ya tatizo lake la jicho kutopata nafuu.

Manara anasumbuliwa na ugonjwa wa macho, huku jicho la kushoto likishindwa kufanya kazi na sasa ameamua kuangalia mbele zaidi.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Manara alisema muda wowote kuanzia leo Jumatatu, anatarajiwa kwenda kati ya Uturuki, Ujerumani au India kwa ajili ya matibabu huku akiwaomba Watanzania kumuombea apone haraka.

 “Wiki ijayo, muda wowote kuanzia kesho (leo), nategemea kwenda nje ya nchini kwa matibabu zaidi. Inaweza kuwa safari ya India, Ujerumani ama Uturuki lakini hiyo yote itategemeana na majibu nitakayopata kutoka hospitalini. Muhimu ni Watanzania kuniombea ili niweze kurejea katika hali yangu ya kawaida,” alisema Manara.

Post a Comment

 
Top