MSANII wa Muziki wa Hip Hop, Miraj Ayoub ‘Mas Stanza’ ambaye sasa anatesa na ngoma yake ya Mwanzo amechekelea baada ya kuona mashabiki wamempokea vizuri.
Mas Stanza anayevutiwa na kazi za rapa Nash MC, alisema hii ni ngoma yake ya tatu kuachia na anadai amefurahishwa na namna mashabiki walivyoupokea wimbo huo ambao ameufanya kwenye studio za Lupaso.
“Nashukuru Mungu mashabiki wangu wameupokea vizuri wimbo wangu, pia kwa upande wa redio zile za mkoani ndiyo zinaonekana kuwa mstari wa mbele kuusapoti, sasa hivi najipanga kwa ajili ya kuanza kufanya video kali itakayonivusha kimataifa,” alisema Mas Stanza.

Post a Comment

 
Top