WAZIRI wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amewataka viongozi wa timu zinazoshiriki Ligi Kuu Bara na Daraja la Kwanza kwenda kuangalia vipaji kwenye Michuano ya Sports Extra Ndondo Cup inayoendelea kwenye Uwanja wa Bandari uliopo jijini Dar.
Nape ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mchezo uliopigwa jana kati ya Goms ambayo ilishinda mabao 2-0 dhidi ya Buguruni alisema amefurahishwa na namna michuano hiyo inavyoendeshwa huku akiwasifia wachezaji wa timu hizo kuwa wamekuwa na vipaji vikubwa.
 “Ninayapongeza mashindano kwa kuwa yanawakutanisha vijana pamoja, naamini yatatoa vipaji vingi  niziombe  klabu za ligi kuu na daraja la kwanza kupitia mabenchi yao ya ufundi waje kuangalia mashindano haya ili wawasajili wachezaji.

Wakati huohuo kuhusiana na kashfa ya rushwa iliyojitokeza kwenye mechi za mwisho za Ligi Daraja la Kwanza Bara, Nape alisema: “Serikali tayari imeunda timu kwa ajili ya kufuatilia hilo na nimekutana na Mkurugenzi wa Takukuru (Valentino Mlowola) ili kuhakikisha suala hilo linapatiwa jibu mapema, kama serikali tunataka kukomesha vitendo vya rushwa na kuukata kabisa ule mzizi wake,” alisema Nape.      

Post a Comment

 
Top