NEYMAR JR yuko kwenye msuguano mkali wa maisha binafsi ndani ya Barcelona, imebainika.
Mshauri wa karibu wa mchezaji huyo, Wagner Ribeiro, alianza wiki hii kwa kusema kwamba klabu tatu kubwa zipo tayari kutoa Euro 200 milion kumnasa Mbrazili huyo.
Klabu hizo ni PSG, Manchester United na Real Madrid zimekuwa zikihusishwa na Neymar tangu  kumalizika kwa msimu huu.
Na imedaiwa kwamba kuna sakata zito ndani ya kambi ya Barca ambalo linamhusisha moja kwa moja Neymar.
"Uhusiano kati ya (Lionel) Messi  na Neymar siyo mzuri. Messi hakubaliana na tabia ya Neymar, wakati Mbrazili huyo haoni jinsi atakavyoweza kushinda tuzo ya Ballon d'Or akiwa na Messi katika timu moja.”
"Pia, uhusiano wake na kocha Luis Enrique ni mbaya zaidi kuliko ule kati yake na Messi..." kimesema chanzo cha ndani ya Barcelona.
Kutokana na hali hiyo, inadaiwa kuwa Neymar ataondoka Barcelona na kuna dalili kubwa kwamba hilo linaweza kutokea kwenye dirisha hili la uhamisho wa majira ya kiangazi.

Pamoja na PSG na Manchester United, Real Madrid imetajwa kuwa kwenye mpango wa kuinasa saini ya fowadi huyo na kuwatishia wapinzani wao hao kwamba, watarudia kile walichowahi kukifanya kwa Luis Figo.
Barcelona yenyewe bado inaamini Neymar atasaini mkataba mpya na kuendelea kubaki kwenye kikosi chao na kuachana na vurugu zote kutoka kwa klabu mbalimbali.
Hata hivyo, inasemwa kuwa jambo hilo si rahisi kama ambavyo Barcelona inavyotarajia.
Wakati giza kuhusu hatima ya staa huyo likiwa kubwa, dada wa staa huyo, mrembo Rafaella amezua utata na kuchochea uvumi kwamba, Neymar ataihama Barcelona kwenye dirisha hili.

Wawakilishi wa klabu za Man United, Real Madrid na PSG wanaripotiwa kukutana na Mbrazili huyo nyumbani kwao Brazil.

Mrembo Rafaella, ambaye ni dada wa Neymar aliweka picha kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuandika maneno ambayo yalichochea uvumi kuhusu fowadi huyo.
Raffaela aliweka picha ya milango miwili ya treni iliyokaribiana sana na kisha kuandika maneno: "Natumaini utakwenda mahali ambako patakufanya uwe na furaha."

Post a Comment

 
Top