Emmanuel Mbaga akijiandaa kusaini mkataba mbele ya viongozi wa Coastal Union.


COASTAL Union ambayo msimu wa 2016/17 itacheza Ligi Daraja la Kwanza baada ya msimu uliopita kushuka, imemsajili kiungo mshambuliaji, Emmanuel Mbaga ‘Samatta’ lakini kubwa ametamba kuirejesha timu hiyo ligi kuu.
Mbaga ambaye amekuwa akivutiwa na nyota wa Tanzania anayechezea Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta amejiunga na kikosi hicho kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea Klabu ya Opec ya visiwani Zanzibar amesema amejiunga na Coastal kwa kuwa anaamini ni sehemu sahihi kwake na kwamba atapambana na wenzake ili kuhakikisha inarejea ligi kuu msimu unaofuata.

Akizungumza na spotiripotablog, Mbaga alisema, mashabiki hawatakiwi kuwa na hofu kwani yeye na wenzake wamejipanga kuhakikisha wanaifanya kazi ambayo imewafikisha sehemu hiyo na wanaamini ligi itaisha kwa furaha.
“Cha muhimu tuombe uzima kwanza kwani ndiyo kila kitu. Lakini niwaahidia mashabiki wetu kuwa mimi pamoja na wenzangu tutapigana kuhakikisha tunairudisha timu ligi kuu, makocha wetu ni wazuri na wamekuwa wakitupa mazoezi mazuri ambayo ndiyo yanayotufanya tujiamini kuwa tutarejea ligi kuu msimu ujao,” alisema Mbaga ‘Samatta’.

Post a Comment

 
Top