KOCHA Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog, amekiri kuwa bado kuna upungufu kwenye safu yake ya ushambuliaji ambayo amepanga kuiimarisha ili wapate ushindi wa mabao mengi kwenye Ligi Kuu Bara.
Safu ya ushambuliaji ya Simba inaundwa na Mrundi, Laudit Mavugo, Muivory Coast Fredric Blagnon, Ibrahim Ajib na Daniel Lyanga.
Tatizo hilo la ushambuliaji, pia Kocha Mkuu wa Yanga Mholanzi, Hans Pluijm amekuwa akililalamikia kutokana na washambuliaji wake, Amissi Tambwe, Donald Ngoma na Obrey Chirwa kushindwa kutumia nafasi nyingi wanazozipata kwenye mechi.
Akizungumza na Championi Jumamosi, Omog alisema idara zote zimekamilika kwenye kikosi chake huku akitaja safu ya ushambuliaji ndiyo yenye upungufu inayohitaji kuboreshwa.
Omog alisema, tatizo hilo ameliona kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya Ndanda FC wiki iliyopita ambayo kama washambuliaji wake wangekuwa makini, basi wangefunga mabao zaidi ya matano.
Aliongeza kuwa, baada ya kugundua upungufu huo, tayari amewapa mbinu mbalimbali za kufunga mabao ikiwemo mashuti ya mita 20 na kumchambua kipa.
“Kikosi changu kipo fiti kila sehemu, lakini tatizo lililopo ni kwenye safu ya ushambuliaji ambayo inahitaji uboreshaji mdogo ili kuhakikisha timu inapata ushindi wa mabao mengi.

“Uzuri, upungufu huo nimeuona mapema na tayari nimeanza kuufanyia baadhi ya marekebisho kuhakikisha washambuliaji wangu wanafunga kila nafasi tutakayoitengeza.
“Kikubwa ninataka washambuliaji wangu wacheze kwa nidhamu kubwa na kutimiza majukumu yao ya kufunga na kutengenezeana nafasi za kufunga,” alisema Omog.

Post a Comment

 
Top