IKICHEZA mchezo wa pili kwenye ligi kuu ya soka Tanzania bara msimu huu, Mbeya City jana imefanikiwa kuvuna pointi zote tatu muhimu baada ya kuifunga Toto Afican ya Mwanza bao 1-0 kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa CCM Kirumba.

Haruna Shamte lifunga bao hilo mapema dakika ya saba kwa mpira wa adhabu iliyotolewa baada ya Joseph Mahundi kuangushwa alipokuwa akijaribu kuwatoka walinzi wa Toto African, hii ilikuwa ni baada ya mashambulizi mfululizo ambayo City iliyafanya kwenye lango la timu hiyo ya Mwanza tangu kipenga cha kuanza mpira  kilipopulizwa.


Raphael Daud, Kenny Ally na Joseph Mahundi walicheza vizuri kwenye eneo la kiungo na kuifanya City kung’ara vizuri uwanjani kipindi chote cha kwanza licha ya jitihada za mara kadhaa kutoka kwa wachezaji wa Toto.

Baada ya mchezo huo kumalizika Kocha wa Mbeya, Kinnah Phiri alisema: “Vijana wangu wameonyesha mchezo mzuri, kama ilivyokuwa kwenye mchezo uliopita, kitu izuri zaidi ni kuwa leo tumepata pointi tatu, hili ni jambo jema, kwa sababu tunapata nguvu ya kupambana kwenye mchezo ujao.”
Mbeya City sasa jumla wamekusanya alama nne kutoka kanda ya ziwa katika michezo miwili waliyoshuka dimbani, awali walitoka sare na Kagera Sugar ambayo inatumia uwanja wa Kambarage, Shinyanga.

Post a Comment

 
Top