KOCHA Mkuu wa Simba, Mcameroon, Joseph Omog, amewapongeza watani wao wa jadi, Yanga, kwa rekodi nzuri waliyoiweka kwenye Kombe la Shirikisho Afrika huku akiitabiria makubwa timu hiyo mwakani kwenye michuano hiyo.
Yanga iliondolewa kwenye michuano hiyo katika hatua ya Nane Bora ya Kombe la Shirikisho Afrika ikiwa na pointi nne.
Omog alisema Yanga ilijitahidi kwa hatua hiyo iliyofikia, hivyo wanastahili pongezi na kikubwa kinachotakiwa kwao ni kujipanga kwa ajili ya mwakani ili wafike mbali zaidi ya hapo walipofikia mwaka huu.

Aliongeza kuwa, ilikuwa ngumu kwa Yanga kusonga mbele zaidi kwenye michuano hiyo kutokana na kundi kushirikisha timu zenye uzoefu kama TP Mazembe ambayo inashiriki kila mwaka.
“Mechi yao na Mazembe, sijajua wamecheza kwa kiwango gani, lakini kikubwa ninawapongeza kwa rekodi nzuri waliyofikia katika michuano hiyo mikubwa Afrika.
“Ninaamini mwakani watafika katika hatua nzuri ya michuano kama hiyo baada ya kupata uzoefu na mbinu zake msimu huu, ilikuwa ngumu kwa Yanga kufika hatua nyingine kutokana na kundi lao kuwepo baadhi ya timu zenye uzoefu kama Mazembe yenyewe ambayo kila mwaka inashiriki,” alisema Omog.

Post a Comment

 
Top