MAVUGO (CHINI) NA KICHUYA

Rais wa Klabu ya Vital’O ya Burundi alikokuwa akichezea straika huyo, Benjamin Bikolimana, amesema wamepokea Sh milioni 80 kutoka klabu ya Simba na wao kiroho safi hawana kinyongo chochote na wamemruhusu kijana wao kwa moyo mweupe kuwatumikia Wana Msimbazi.

“Tuna uhusiano mzuri na Simba tangu zamani hivyo licha ya kutaja kiasi cha Sh milioni 200 ambazo tulizitaka awali, alikuja kiongozi wao mmoja tukakaa naye mezani na kukubali kushusha hadi milioni 80 ambazo wameshalipa, hivyo kwa sasa  hatuna tatizo nao.

“Tumemruhusu kijana wetu kwa moyo mmoja, tunajua huko Tanzania amekuja kufanya kazi, kama atapewa ushirikiano nina imani mashabiki wa Simba watafurahi wenyewe,” alisema.

Post a Comment

 
Top