BAADA ya kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya African Lyon, kikosi cha mabingwa wa soka Afrika Mashariki na Kati Azam FC, leo kimefanya mazoezi mepesi ya kurudisha mwili kwenye hali yake leo kwa wachezaji waliocheza dakika zaidi ya 45 kwenye mchezo wa jana dhidi ya Afrika Lyon.


Wachezaji wengine ambao hawakupata muda mrefu wa kucheza na wale ambao hawakucheza kabisa, wenyewe waliendelea na mazoezi ya kawaida ili kujiweka fiti.


Post a Comment

 
Top