DIDA AKIWA LANGONI KATIKA MCHEZO WA LEO DHIDI YA AFRICAN LYON

BABA mzazi wa kipa namba moja wa Yanga, Deogratius Munish, Boniventure Munish amefariki leo mchana.
Habari tulizozipata zinasema baba huyo alifariki  leo mchana huku DIda akiwa uwanjani leo kuivaa Lyon ambapo walishinda mabao 3-0.
Inaripotiwa kuwa baba huyo ambaye alikuwa akisumbuliwa na homa kwa muda mrefu alipooza upande wa mwili ambapo mara ya mwisho alipeleka Hospitali ya Ocean Road jijini Dar.
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi! Msiba utakua Mikoroshini jijini Dar.

Post a Comment

 
Top