STAA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ni kama ameamua kujibu mapingo kwa kocha wake wa zamani, Jose Mourinho kupitia mtandao wa Instagram.
Mourinho ambaye kwa sasa ni kocha wa Manchester United alimponda Ronaldo kwa kitendo chake cha kutoa maelekezo kwenye mchezo wa fainali wa Kombe la Euro katika kipindi cha dakika za nyongoze.
Ronaldo aliumia mapema tu kwenye mchezo huo wa fainali dhidi ya Ufaransa, lakini wakati wa dakika 30 za nyongeza alisogea kwenye mstari wa makocha na kuanza kuwapa wachezaji wenzake maelekezo tukio ambalo Mourinho aliliponda na kusema wala halikuwasaidia Ureno kutwaa ubingwa huo.
Hata hivyo, wikiendi iliyopita Ronaldo aliweka picha kwenye mtandao wa Instagram akiwa na Bruno Alves, Pepe, Andre Gomes wakisherehekea ubingwa huo wa Euro na kuandika 'Nakumbushia Mapema',.
Picha hiyo ilipata komenti nyingi zilizoonyesha kuwa Ronaldo alikuwa akimjibu Mourinho.
“Cristiano Ronaldo hakuisaidia timu, kulikuwa na wachezaji 11 uwanjani ambao walikuwa wakifanya kazi yao lakini siyo Ronaldo.
“Mtu aliyekuwa kwenye benchi akifundisha timu ni kocha siyo Ronaldo, nilimuona kama mtu aliyeshindwa kujizuia,” alisema Mourinho siku chache zilizopita.

Post a Comment

 
Top