BAADA ya kikosi cha Kagera Sugar kinachoshiriki Ligi Kuu Bara kukubali kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Alliance kwenye mchezo wa kirafiki uliopigwa Uwanja wa Butimba TTC, kocha mkuu wa hiyo, Mecky Mexime amesema bado kikosi chake kinajiandaa na kitakuwa fiti kabla ya ligi kuanza.

Kagera Sugar ipo mkoani hapa kwa ajili ya michezo kadhaa ya kirafiki na timu zinazoshiriki Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Kuu zilizopo ili kuimarisha kikosi cha timu hiyo.

Mexime alisema pamoja na kupoteza mchezo huo bado anaimani na kikosi chake kuwa kitafanya vyema msimu ujao kwenye ligi kuu.

"Tumekuja Mwanza kwa ajili ya kucheza michezo kadhaa ya kirafiki na timu zinazoshiriki daraja la kwanza na ligi kuu ili kuangalia upungufu mapema kabla ligi haijaanza kupoteza mchezo wetu dhidi ya Alliance hilo kwetu hatuoni shida bali upungufu  uliojitokeza ndiyo tutakaoufanyia kazi mapema,” alisema Mexime.

Post a Comment

 
Top