![]() |
|
Anita
na mchepuko
|
SIRI
imefichuka kuwa staa wa Liverpool, Dejan Lovren, hakwenda kwenye michuano ya
Euro mwaka huu ili kuilinda ndoa yake.
Mchezaji
huyo mwenye uraia wa Croatia aliamua kutokwenda kwenye michuano hiyo baada ya
kugundua kuwa mke wake anayejulikana kwa jina la Anita, ana uhusiano na rafiki
wake wa zamani anayejulikana kwa jina la Dario Torbic, 26.
Mke
huyo na mume tayari wana watoto wawili.
Inaelezwa
kuwa wawili hao walikuwa wanajiandaa kuachana na beki huyo alikuwa lazima
afanya kitu ili hali hiyo isitokee.
Uhusiano
wa beki Dario na mke wa beki huyo ulianza mwezi Desemba mwaka jana wakati wawili hao walipokutana mjini Zagreb.
Hata
hivyo, inaelezwa kuwa Anita alimwambia Dario aende England na wakakutana kwenye
hoteli ya Liverpool.
Hata
hivyo, inaelezwa kuwa Lovren alifahamu mchezo huo na wawili hao waliondoka
England mwezi Machi kwa ajili ya kwenye Croatia kuonana na mwanasheria ili
kufanya utaratibu wa talaka.
Chanzo
kilisema: “Ndoa ya Dejan Anita imekuwa kwenye majaribu makubwa sana kwa muda
mrefu huko rafiki wa Lovren akihusishwa na taarifa za kutembea na mwanadada
huyo.
“Anita alimwambia mwanaume huyo kuwa
wanakwenda Croatia kwa ajili ya talaka na baada ya hapo watakuwa wakiishi
pamoja.
“Lakini
tukio hilo lilishindikana kutokana na Anita kuwa mjamzito ndipo Dejan akaamua kupambana
na ndoa yake, na kupanga kuwa mwezi Juni anatakiwa kupumzika na mke wake ili
kupata suluhisho la matatizo yote jambo ambalo mkewe aliliridhia.”
Inaelezwa
kuwa alijitoa kwenye timu ya taifa bila kutoa taarifa yoyote na mwisho
aliondolewa kwenye timu hiyo na kuweka chuki kwa mashabiki wa Croatia ambao
walikuwa wakimtegemea.



Post a Comment