Mechi ya kirafiki kati ya Azam FC dhidi ya URA ya Uganda ambayo inatarajiwa kupigwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex utapigwa saa 1:00 Usiku badala ya saa 10:oo Jioni kama ilivyokuwa awali.
Viingilio kwenye mchezo huo vitakuwa Sh 1,000 kwa viti vya kawaida na 3,000 kwa viti maalumu (V.I.P).
Azam FC inapenda kuwakaribisha mashabiki wote wa soka kuhudhuria mchezo huo unaotarajia kuwa mkali na wa aina yake utakaopambwa na burudani safi kutokana na ubora wa vikosi vyote viwili vinavyocheza soka la kitabuni.

Post a Comment

 
Top