YANGA
sikieni salamu zenu kutoka kwa mbaya wa mabeki wa timu pinzani, Laudit Mavugo
raia huyo wa Burundi amesema amejipanga ipasavyo katika kuisaidia timu yake hiyo
kufanya vizuri msimu ujao.
Mavugo
amesajiliwa Simba msimu huu akitokea Vital’O ya Burundi ambapo hadi sasa
amefanikiwa kufunga bao moja katika mechi ya Simba Day, hali ambayo imeamsha
hamasa kwa mashabiki wa timu hiyo.
Amesema
hawezi kuogopa mabeki wa Yanga siku watakayokutana na timu hiyo katika michuano
ya Ligi Kuu Bara msimu ujao unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Agosti 20, mwaka
huu.
“Naijua
vizuri Yanga, nimewahi kukutana na mabeki wao kama Cannavaro (Nadir Haroub),
Kelvin Yondani, hawawezi kunipa tabu na katika utaratibu wa maisha yangu huwa
siogopi mtu, nitapambana nao tu. Naweza kuwapenya na nikafanya maajabu,”
alisema kipenzi huyo cha mashabiki wa Simba.



Post a Comment