MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji, ameibuka upya baada
ya juzi kutangaza kutaka kuikodi klabu hiyo kwa muda wa miaka kumi ili kuifanya
kuja kuwa moja ya klabu kubwa ndani na nje ya nchi.
Juzi Jumamosi Yanga ilifanya Mkutano Mkuu wa Dharura kwa
wanachama wa klabu hiyo ambapo Manji alitangaza ombi lake hilo ambalo sasa kazi
imebaki kwa Baraza la Wadhamini la Klabu ya Yanga kukubali au la.
“Unajua Yanga ina thamani kubwa kuliko hata fedha
nilizokuwa nazo na naamini hakuna tajiri ambaye atakuja kuinunua Yanga kwa
sababu ina thamani kubwa na ndiyo maana nimesema siwezi kutaja kiasi cha fedha
ambacho nitakitoa kuikodi bali nitakachokifanya ni makubaliano na Baraza la
Wadhamini kwa yale ambayo nimeyapanga ikiwemo hizo asilimia 25 za faida kuingia
klabuni.”


Post a Comment