KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Shiza Kichuya, ameweka bayana kuwa licha ya kuonyesha uwezo wa hali ya juu katika mchezo dhidi ya AFC Leopards ya Kenya, Jumatatu ya wiki hii, kwake yeye anaona bado ana mambo mengi ambayo amedhamiria kuyafanya akiwa na uzi wa Simba.

Kichuya ambaye amejiunga na Simba hivi karibuni akitokea Mtibwa Sugar, alikuwa moto katika mchezo wa timu hiyo uliopigwa juzi Jumatatu katika Uwanja wa Taifa, Dar dhidi ya AFC Leopards ambapo alihusika kwenye mabao matatu ya timu hiyo ya Ibrahim Ajibu na Laudit Mavugo huku akifunga bao moja.

Kichuya anayemudu kutumia vema mguu wa kushoto, ameliambia Championi Ijumaa kuwa nia yake tangu alipotua ndani ya timu hiyo ni kuona anaipa mataji kwa kuonyesha kiwango cha hali ya juu katika kila mchezo wa timu hiyo.

“Nachokifanya mimi ni kuonyesha uwezo na kupambana katika kila mchezo wetu kwani nimepania kuipa mataji timu yangu hii na ili kutekeleza ahadi hiyo, ni lazima niweze kujituma katika kila mchezo wetu, uwe wa kirafiki au ligi.

“Hapa mbona bado kabisa sijaonyesha cheche zangu na hata robo bado sijafika, nachotaka kukifanya kwa msimu huu watu hawataamini, cha msingi wao waendelee kunitazama katika kila mchezo wetu nini ambacho nitakuwa nakifanya,” alisema Kichuya.

Post a Comment

 
Top