KOCHA wa
Arsenal, ARsene Wenger ameonekana kulichukulia kwa umakini mkubwa suala la
usajili wa mlinzi wa kati baada ya kuripotiwa kuwa klabu yake imefikia
makubaliano binafsi ya kumsajili beki wa Valencia, Shkodran Mustafi.
Arsenal sasa
inahaha kupata mlinzi wa kati atakayeziba nafasi ya Per Mertesacker na Gabriel Paulista
ambao wameumia na wanatarajiwa kuwa nje kwa ziadi ya miezi mine kila mmoja.
Baada ya
kutumia siku mbili kwaajili ya mazungumzo juu ya dili la mchezaji huyo,
hatimaye wakala waa Mustafi amethibitisha kwamba dili sasa lipo mbioni
kukamilika, huku Arsenal wakitakiwa kumalizana na klabu ikiwa ndiyo hatua ya
mwisho.
"Shkodran
na Arsenal wamefikia makubaliano, hatua iliyobaki ni Arsenal kumalizana na
klabu yake ," Ali Bulut amesema ambaye ni wakala wa Mustafi.
Post a Comment