LAUDIT
Mavugo asicheze Simba? Haiwezekani, kwa sababu tayari uongozi wa miamba hiyo ya
Msimbazi umejipanga kupambana kuhakikisha straika huyo Mrundi anakuwa sehemu ya
kikosi cha Joseph Omog kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania
Bara.
Kumekuwa na
taarifa zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ambazo zimekuwa zikidai kuwa
Mavugo hawezi kucheza Simba msimu ujao kwa sababu bado ana mkataba na klabu
yake ya Vital’O ya Burundi, lakini uongozi wa Simba umefunguka na kudai kuwa
iwe isiwe lazima staa huyo avae jezi zao msimu ujao.
Akizungumza
na BINGWA jana Katibu Mkuu wa Simba, Patrick Kahemele, alisema kwa sasa wapo
kwenye mazungumzo na Vital’O kwa ajili ya kukamilisha usajili wa straika huyo
ambaye tayari amekuwa kipenzi cha mashabiki wa Msimbazi.
Kahemele
alisema tayari hatua ya kwanza katika usajili wa staa huyo imeshakamilika kwa
makubaliano ya pande mbili kati ya klabu na mchezaji na kinachosubiriwa sasa ni
hatua ya pili ya makubaliano ya klabu na baadaye kutumiwa Hati ya Uhamisho wa
Kimataifa (ITC).
Katika hatua
nyingine, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji Simba ambaye hakutaka jina lake litajwe
gazetini, alisema hata kama Vital’O wakigoma kutuma ITC kwa muda mwafaka
watapiga hodi kwa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ili kupata kibali cha
kumchezesha Mavugo.
“Kuna
kipengele Fifa ambacho kinaruhusu mtu kupewa kibali cha muda ndani ya siku 14
kama klabu yake ikigoma kutuma ITC, hivyo kama Vital’O wakigoma basi tutaenda
hatua inayofuata kuhakikisha Mavugo anacheza Msimbazi msimu ujao,” alisema.
Akizungumzia
sakata hilo la usajili kwa upande wake Rais wa klabu ya Vital’O, Bikolimana
Benjamin, ametoa kauli ambazo zinaweza kuishangaza Yanga ambayo kipindi fulani
iliwahi kutajwa kumfukuzia kimya kimya Mavugo baada ya kudai kuwa timu yake iko
tayari hata kuwaazima Simba straika huyo.
“Sisi na
Simba hatuna tatizo lolote hivyo hata kama wakishindwa kutoa fedha tunaweza
kuwaazima mchezaji wakamtumia kwa mwaka mmoja na baadaye akarudi Vital’O.
“Siwezi
kutaja fedha yoyote ile viongozi wa Simba wanajua nini kinaendelea na kuhusu
mkataba ni kweli kuwa bado Mavugo ana mkataba na sisi ila siwezi kusema
unamalizika, lakini Simba wanajua,” alisema.
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.