JOTO la mechi ya Ngao ya Jamii kati ya Azam na Yanga linazidi kupanda, baada ya kocha wa Azam, Zeben Hernandez, kusema nguvu zake zote anaelekeza katika pambano hilo litakalochezwa Agosti 17 mwaka huu, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mechi hiyo itakuwa ya kwanza kwa Hernandez kucheza na Yanga aliyeanza kuifundisha Azam baada ya aliyemtangulia, Stewart Hall kuachia ngazi.


Azam kabla ya kuvaana na Yanga  wanatarajia kujipima nguvu kwa URA ya Uganda katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na BINGWA jana, Hernandez alisema mechi hiyo itakuwa ya mwisho ya kirafiki kabla ya kukutana na Yanga kwenye mechi ya kuashiria ufunguzi wa msimu mpya Ligi Kuu Bara.

“Mechi yetu na URA itakuwa ni kipimo tosha kwa ajili ya kupambana na Yanga,  kwani mawazo yangu ni kushinda na kutwaa Ngao ya Jamii,” alisema Hernandez.

URA ilimaliza katika nafasi ya tano katika Ligi Kuu ya Uganda kutokana na pointi 47, huku Azam ilishika nafasi ya pili Ligi Kuu Bara.

Post a Comment

 
Top