MENEJA wa Juventus, Massimiliano Allegri amemtaka kiungo wake, Paul Pogba ambaye anatakiwa na Man United kurejea haraka kikosini kesho Jumatatu tayari kwa kuanza mazoezi na wenzake.

Mchezaji huyo raia wa Ufaransa tangu ilipomalizika michuano ya Euro 2016 alikuwa mapumzikoni akila bata huko Marekani.


Pogba, 23, amekuwa akihusishwa na kuhamia Old Trafford kwa bei ya kuvunja rekodi ya dunia ya ununuzi wa wachezaji ya pauni milioni 100.

Meneja wa United, Jose Mourinho aliwahi kusema klabu yake imekaribia kumsaini kiungo huyo lakini mpaka sasa zimebaki tetesi tu!
"Kwa sasa, Pogba ni mchezaji wa Juventus," amesema Allegri.

Post a Comment

 
Top