April 7, 2025 11:10:05 AM Menu




ARSENAL inajipanga kwa vita na Everton katika kuwania saini ya beki wa kati wa Swansea, Ashley Williams, ambaye dau lake linatajwa kuwa pauni milioni 10. Arsenal pia imetajwa pia kutenga pauni milioni 15 kwa ajili ya kumsaini beki wa West Brom, Jonny Evans, 28.

Sunderland
KOCHA mpya wa Sunderland, David Moyes anataka kuwasjaili nyota aliokuwa nao Man United, kiungo Marouane Fellaini na Adnan Januzaj.

Roma
ROMA imeongeza kasi ya kutaka kupata saini ya beki wa Manchester United, Matteo Darmian baada ya walinzi wake, Mario Rui na Antonio Rudiger kuumia hivi karibuni.

West Ham
WEST Ham inajipanga kutoa ofa ya pauni milioni 20 ili ipate ridhaa ya kumsajili mshambuliaji wa Swansea City, Andre Ayew, baada ya ile ya kwanza ya pauni milioni 16 kukataliwa.

Man City
MANCHESTER City inakaribia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa Schalke, Leroy Sane baada ya kukubali kutoa dau ya pauni milioni 31.2.

Chelsea
MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte anaamini klabu yake itamsajili tena aliyekuwa mshambuliaji wa kikosi hicho, Romelu Lukaku, 23, kutoka Everton. Blues wamepanga kutoa ofa ya pauni milioni 60.


Arsenal
ARSENAL wamepanga kumtengea pauni milioni 50 straika wa Inter Milan, Mauro Icardi, 23, ikiwa watashindwa kukamilisha dili la mshambuliaji wa Lyon, Alexandre Lacazette, 25.

Galatasaray
KIUNGO wa Liverpool, Lucas Leiva, 29, anatarajiwa kukamilisha dili la kujiunga na Galatasaray ya Uturuki kwa dau la pauni milioni 2.3 wiki hii.

Man United
KOCHA wa Manchester United, Jose Mourinho anataka kumsajili beki wa kati mwenye uzoefu kikosini humo ili kuongeza nguvu msimu ujao. Pia beki wa Chelsea, Baba Rahman, 22, anatarajiwa kujiunga na Schalke kwa mkopo wa muda mrefu.

01 Aug 2016

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top