CALIFORNIA, Marekani
MCHEZAJI wa kikapu, DeMar DeRozan ambaye kwa sasa ni mchezaji huru, imeelezwa kuwa amekubali kurejea kwenye timu ya Toronto Raptors na kusaini mkataba wa miaka mitano wenye thamani ya dola milioni 139.

DeRozan alikuwa katika timu hiyo inayoshiriki ligi ya kikapu ya NBA tangu mwaka 2009 lakini alimaliza mkataba na kuwa mchezaji huru baada ya msimu wa 2015/16 kufikia tamati lakini kuna uwezekano mkubwa wa kurejea katika timu hiyo.

Msimu uliopita DeRozan alikuwa na wastani wa pointi 23.5 katika mechi 78 alizocheza.

Toronto haikuwa na msimu mzuri japokuwa ilifika hatua ya fainali ya Ukanda wa Mashariki na kutolewa na Cleveland Cavaliers ambao baadaye walifanikiwa kuwa mabingwa.

Taarifa zinasema kuwa DeRozan atatambulishwa rasmi Julai 7, mwaka huu kuwa mchezaji wa Raptors.

Post a Comment

 
Top