PARIS, Ufaransa
BEKI wa timu ya taifa ya Ufaransa, Patrice Evra amesema kuwa wao watakuwa makini na hawataidharau Iceland kama ilivyotokea kwa England katika michuano ya Euro inayoendelea.

Ufaransa inatarajiwa kucheza dhidi ya Iceland, leo Jumapili katika nusu fainali ya michuano hiyo huku wengi wakiipa nafasi Ufaransa kupata ushindi. Iceland walifika hatua hiyo baada ya kuifunga England mabao 2-1 katika robo fainali, wiki iliyopita.

Beki huyo wa zamani wa Manchester United amesisitiza kuwa England hawakuiheshimu Iceland na ndiyo maana wakapoteza mchezo huo.

“Inanipa hofu kwa kuwa England hawakuiheshimu Iceland kwa kuwa watu wengi wanadharau mataifa madogo,” alisema beki huyo mwenye umri wa miaka 35.


“Kilichotokea England walitakiwa kushinda lakini kwa kawaida unapoingia katika mchezo unatakiwa ujiwekee asilimia 50-50.

“Mara baada ya mechi yetu dhidi ya Ireland kuna Waingereza wakawa wananiuliza juu ya mimi kukutana na England lakini nikawajibu kuwa chochote kinaweza kutokea katika mchezo wao na Iceland lakini hawakulijali hilo,” alisema Evra

Post a Comment

 
Top