April 11, 2025 03:34:06 AM Menu




 WAKATI Simba ikiendelea na kasi yake ya kuzifunga timu zinazowasogelea, taarifa njema kwa mashabiki wao ni kwamba, taratibu za kumrudisha nchini Emmanuel Okwi zinakwenda vizuri.

Okwi, ambaye ni kipenzi cha mashabiki wa Simba, anaichezea SonderjykE ya nchini Denmark, lakini Wekundu hao wa Msimbazi wanafanya juhudi kubwa za kumrejesha ambapo hata mchezaji mwenyewe ameonyesha nia, jambo ambalo linawapa wepesi Simba.

Taarifa kutoka Simba zinadai kuwa, kuna vigogo wawili wenye ushawishi mkubwa ndani ya Wekundu hao wa Msimbazi wametumwa nchini Denmark kukutana na Okwi na waajiri wake.


Katika timu hiyo, Okwi amekuwa hapati namba, ndiyo maana naye ameona bora arejee kwenye timu yake na viongozi wa Simba wanafanya kila linalowezekana ili kukamilisha zoezi hilo.

Katika hatua nyingine, wakati harakati hizo zikiendelea, taarifa nyingine zinadai kuwa, wanamfuatilia kwa ukaribu mshambuliaji wa zamani wa Azam FC, Kipre Tchetche, anayekipiga nchini Oman.

Kama dili hilo likitiki, Wekundu hao wakafanikiwa kumrejesha Okwi, pia wakainasa saini ya Kipre, Simba itakuwa moto wa kuotea mbali.

02 Nov 2016

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top