April 11, 2025 04:32:06 AM Menu




KOCHA Mkuu wa Yanga Mzambia, George Lwandamina amembadilishia majukumu mshambuliaji wake, Juma Mahadhi kwenye kikosi hicho.
Hiyo, ikiwa ni wiki moja tangu kocha huyo aanze kukinoa kikosi hicho kinachojiandaa na mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara utakaoanza Jumamosi ijayo.
Kocha huyo, hivi sasa yupo katika mipango thabiti ya kukiboresha kikosi chake ili kuhakikisha anapata wachezaji 11 watakaokuwa wanaanza.
Mzambia huyo, kwenye mechi ya wikiendi iliyopita na JKU alimchezesha Mahadhi namba nane, nafasi inayochezwa kwenye timu hiyo na Mnyarwanda, Haruna Niyonzima na Mzimbabwe, Thaban Kamusoko.
Katika mechi hiyo iliyomalizika kwa Yanga kufungwa mabao 2-0 yote yakifungwa kipindi cha kwanza, Mahadhi alionyesha umahiri wa kuchezesha timu na kukaa na mpira huku akipiga pasi safi kwa wachezaji wenzake.
Mshambuliaji huyo, alicheza katika nafasi hiyo kwa dakika 45 za mchezo huo, kabla ya kipindi cha kutolewa na nafasi yake ikachukuliwa na Kamusoko.
Akizungumzia hilo, Lwandamina alisema: "Hivi sasa ninatengeneza kikosi cha kwanza nitakachokitumia kwenye mzunguko wa pili wa ligi kuu, hivyo ni lazima nimjaribu kila mchezaji ili nione uwezo wake.”

14 Dec 2016

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top